Cover Image
close this bookUtenzi wa Nyakiiru Kibi (ECOL Publications, 1997, 109 p.)
View the document(introduction...)
View the documentKutabaruku
View the documentDibaji
View the documentFasilu ya Kwanza
View the documentFasilu ya Pili
View the documentFasilu ya Tatu
View the documentFahirisi
View the documentKinyume

Fahirisi

Maneno ya Kihaya na lugha nyingine za asili

Ubeti

Neno

Maelezo

13

Ruhanga

Mungu Mkuu, Muumba.

27

Kintu

Mwanamume wa kwanza kwa mujibu wa imani za baadhi ya watu waishio mkoa wa Kagera na Uganda ya Kusini.

28

Kikazi

Mwanamke wa kwanza, mke wake Kintu.

31

Mugasha

Muungu wa Ziwa Viktoria, na mtawala wa tufani, mvua, kwa mujibu wadini zajadi katika mikoa ya Kagera, Mwanza na Kusini mwa Uganda. Wasukuma humwita Nyangassa, Wakerewe humwita Mugasa na Waganda humwita Mukasa.

32

Ngassa

(Kisukuma) Nyangassa, Mugasha.

Mukasa

(Kiganda) Mugasha.

33

Nyanja

Nyanza, Ziwa au mto.

Lweru

Ziwa Viktoria.

35

Nyakalembe

Mke wa Mugasha na Muungu wa kilimo kadka dini za jadi.

36

Kasana

Muungu wa uwindaji.

37

Irungu

Muungu wa mapori na uwindaji.

38

Lyangombe

Muungu wa wafugaji.

39

Kaihura-Nkuba

Muungu waradi, mwanawe Mugasha.

40

Wamala

Muungu Kiongozi wa Wachwezi.

Wachwezi

Kundi la Miungu na Mizimu, hususan lile linalohusishwa na Wamala kiukoo.

Huyamala

Huyamaliza.

41

Kagoro

Mtoto wa Wamala, Muungu wa vita.

42

Kilo

Muungu wa usiku.

43

Kasi

Muungu wa kike anayehusika na kilimo.


Rugila

Muungu wa kike anayehusika na uzazi.

59

Mukama

Mfalme, sultani.


Bike

Mtawala wajadi wa Kiziba aliyeuawa na Ntumwa, labda kwenye karne ya 15.

78

Nanga

Ala ya muziki yenye nyuzi saba na umbo kama la mtumbwi.

89

Ngisha

Hirizi.

96

Katonda

Mungu, Muumba.

104

Ukama

Ufalme.

129

Mshonge

Nyumba ya jadi ya Wahaya, Wachaga, naWaganda, ambayo paa lake huteremka mpaka ardhini; haina kuta za udongo au matofali.

133

Kanwa

Mdomo, kinywa.

Matoke

Ndizi zilizopikwa.

139

Kukaga

Kuhisi, kutambua.

144

Ugino

Ufizi.

171

Wazana

Abazana, watumwa wa kike. Mmoja ni muzana.

175

Bami

Machifu au wazee wenye heshima. Mmojani mwami.

178

Habuka

Neno litumikalo kumsalimu mfalme, maana yake kama dhihirika au tokea hadharani.

Lugaba

Mtoaji wa fadhila, mkarimu.

181

Wakazi

Bakazi, wanawake. Mmoja ni mukazi.

199

Ukazi

Hali ya kuwa mwanamke.

203

Mizio

Miziro, miiko.

230

Kanyamaishwa

Jina lenye maana yamtoto aliyeokotwa porini kama mnyama.

247

Kachwankizi

Jina la ngoma ya utawala wa Kiziba ambayo Nyakiiru alikuja nayo kutoka Bunyoro.

249

Kyezailwe

Jina la ngoma lenye maana ya Kilichozaliwa.

250

Kalemaitalula

Ngoma ya utawala. Maana yake haibebeki.

251

Nyabatama

Jina la ngoma, maana yake haikupatikana.


Matama

Mashavu.

252

Tabamulibi

Jina la ngoma ya utawala lenye maana ya Asiyekosa Soko, Anayehitajika Wakati Wote.

261

Mihango

Amri za mfalme au Mungu.

286

Balangila

Wana wa mfalme. Mmoja ni Mulangila.

302

Katikiro

Waziri Mkuu.

357

Anakomaga

Anatengeneza nguo za milumba.

Nyumanju

Nyuma ya nyumba.

361

Mbugu

Milumba, nguo za magamba ya miti.

371

Kukama

Kukamua.

520

Zinajipogoa

Vichane vya ndizi vinakongoloka vyenyewe.

526

Saza

(Kiganda) Jimbo.

529

Mbito

Wa Ukoo wa Babito. Watawala wa ufalme wa Bunyoro na Kiziba.

543

Mtelele

Tambarare.

597

Nsi

Nchi kavu.

602

Wanyamahanga

Wageni kutoka mbali.

621

Kuyu (nkuyu)

Aina ya samaki wa ziwani.

658

Maka

Kaya.

664

Kikaleni

Katika Kikale, yaani Ikulu.

683

Nyamuhanga

Mungu - Jua.

712

Mihi

Vifaa vya ukili vya kubebea senene wakisha kamatwa. Kimoja ni muhi.

713

Topito

Manati.

732

Watote

Walowe.

798

Kukukuza

Kukuua hutumika kwa mfalme tu.

855

Kutukinda

Kutuchinja, kutuua.

Maneno magumu au matumizi magumu ya maneno

Ubeti

Neno

Maelezo

0

Fasilu

Sehemu, sura.

1

Hisitoria

Historia.

3

Wahenga

Wazee wa kale, watangulizi.

6

Wavyele

Wazazi.

7

Pasina

Pasipo.

Jadi

Asili ya mtu.

8

Ufalume

Ufalme.

9

Elufu

Elfu.

10

Walisakini

Walikaa, waliishi.

12

Wali

Walikuwa.

Miungu

Mizimu.

Mizimu

Pepo za watu waliokwisha kufa.

Mahoka

Pepo za watu waliokwisha kufa.

15

Waafirika

Waafrika.


Kwangamia

Kuangamia.

16

Kuzimuni

Makao ya wafu au mizimu.

Auni

Misaada.

19

Hako

Hayuko.

22

Kwelezawe

Kueleza wake.

23

Umbile

Vilivyoumbwa.

24

Malikia

Malkia.

25

Tufani

Upepo unaovuma kwa nguvu sana.

26

Kuzawana

Kuzaliwa pamoja naye.

30

Ali

Alikuwa.

31

Anafurusha

Anarusha.

34

Mtetemo

Tetemeko la ardhi.

36

Aridhi

Ardhi.

41

Mahiri

Bingwa, mjuzi.

Chuku

Udanganyifu, ulaghai.

42

Humpiku

Humshindi.

44

Walihimidiwa

Waliabudiwa.

45

Ezi

Enzi.

46

Kutongoa

Kuimba, kusimulia.

Kunga

Siri za utunzi.

Mahadhi ya halua

Sauti tamu ya wimbo.

47

Kuhadithi

Kuhadithia.

Uhabithi

Uovu, ubaya.

50

Matetano mzomzo

Magomvi tele.

52

Kasheshe

Fujo, vurugu.

53

Waume wa miraba

Wanaume wakubwa, wenye nguvu.

54

Kuwanda

Kuwa na neema, kustawi.

Kutanda

Kuenea, kuzagaa.

Murua

Nzuri sana.

55

Sulutani

Sultani, mfalme.

56

Kumaizi

Kufahamu.

57

Uzinzani

Uzinza, nchi ya Wazinza.

58

Maliki

Mfalme.

Miliki

Utawala, ufalme.

59

Wadhifa

Cheo.

63

Yali

Ilikiwa.

64

Masogora

Mafundi wa kuwamba ngoma.

66

Tambo

Wakubwa.

Kiambo

Kitongoji, makazi.

68

Ziwa lahema

Ziwa lapandisha nakushusha mawimbi yake.

Kaskazi

Kaskazini.

70

Kufuma

Kutoboa kitu.

Husuma

Chuki.

Hujuma

Shambulizi, uharibifu.

72

Ngwamba

Kazi ngumu.

74

Mzito mja

Mjamzito.

76

Nadhifu

Mzuri, anayevutia.

78

Yakerereze

Yapigekwa msisitizo.

80

Zikatangaa

Zikaenea.

81

Pukupuku

Kwa wingi.

82

Aso makamu

Asiye na umri mkubwa.

84

Kwa tuwatuwa

Kwa kusitasita.

85

Akikita batobato

Akibamiza miguu kama bata.

87

Linayumkini

Linafaa, linastahili.

88

Janga

Maafa.

90

Afia

Afya.

Waa

Doa, dosari.

Asiyechelea

Asiyeogopa.

91

Ahodhi

Amiliki.

92

Zisilitindike

Zisipungue.

95

Myezi

Miezi.

102

Labuda

Labda.

104

Hadhari

Uangalifu.

Liso

Lisilo.

Dhila

Dhara, ubaya.

105

Wakanipalia

Wakinipa.

109

Katu

Kamwe, hata kidogo.

112

Kuzikoroga kwato

Kuja haraka haraka.

114

Mahiri

Hodari, mwenye ujuzi.

115

Hakuita

Nimekuita.

116

Kabula

Kabla

117

Kuikidhi

Kuitimiza.

120

Dhidi

Kupinga.

122

Mtokoto

Mkali, unaotokota.

125

Thawabu

Ahsante, shukrani, zawadi.

128

Tasihili

Kwa haraka.

Tunguri

Vibuyu vidogo vya uganga.

Kili

Ukindu.

131

Kasabahi

Kaamukia, katoa salamu ya asubuhi.

Afua

Uzima, uponaji.

132

Kanagiza

Kaniagizia.

Kuzinuizia

Kuzisalia, kuzisemea maneno ya uganga.

134

Yabisi

Ngumu.

135

Panyiza

Fanya.

137

Kishapo

Kisha hapo.

138

Makeke

Machachari, hekaheka, fujo.

141

Kudhalilisha

Kupunguza nguvu au hadhi.

142

Kutobanga

Kuvuruga.

144

Iso kifano

Isiyo kifani.

146

Kafanza

Kafanyiza, katengeneza.

148

Kutangaa

Kutajika kila mahali, kuzagaa.

149

Sudi

Bahati njema.

150

Kamuengeza

Kambembeleza.

151

Kajipangusha

Kajipangusa.

155

Mikiki

Tendo la kutumia nguvu.

157

Hayajangia

Hayajaingia, hayajaota.

160

Laana

Balaa inayotokana na kukosa radhiya Mungu.

Kitwana

Mtumishi wa kiume aliye kama nusu mtumwa.

Kwambua

Kuambulia; kukutwa najambo.

162

Kwangamia

Kuangamia.

163

Ulozi

Uchawi.

164

Kafi

Kasia la kuendeshea mtumbwi; Mugasha ni Muungu wa ziwa, hivyo inasemekana huonekana akitembea huku ameshika kasia.

Ghafi kanda

Mabaya, maovu, kenea.

Kuwanda

Kuwa nene.

166

Debe shinda

Debe tupu.

Panda

Parapanda, baragumu.

167

Baa

Balaa

168

Kasirini

Ikuluni.

170

Fadhaa

Mshtuko.

171

Kukongolewa

Kuopolewa, kukatwakatwa.

Kengewa

Aina ya mwewe.

172

Kulalama

Kulaani.

175

Harara

Mbio, haraka.

Ghera

Hamu, nia.

176

Ada

Desturi.

Jamala

Fadhila, wema.

177

Malika

Maliki, mfalme.

180

Nafusi

Nafsi.

183

Shari

Rabsha, vurugu.

Watakasiri

Watakasirika.


Wataihasiri

Wataiharibu.

184

Wajihi

Uso, sura.

Hutumika wakad wa kuzungumzia mfalme, mathalan kufika wajihi ni kufika mbele ya mfalme.

185

Pulikeni

Sikilizeni.

187

Naugulia

Nalilia.

Ulezi

Kulea.

Vijaluba

Vifuko.

188

Macho yanasinasina

Machozi yataka kutoka.

Wakajiondokelea

Wakaondoka.

191

Kungia

Kuingia.

194

Tunutu

Mtoto wa nyuki.

196

Huba

Hamu.

199

Ajizi

Usiri, ugumu wa kufanyajambo.

202

Midhana

Balaa.

204

Mwanondolea

Mwaniondolea.

206

Utuvu

Utulivu.

207

Kakata

Kwa mikiki.

Aguta

Anahema.

213

Wakamgura

Wakamuacha.

214

Msito

Kusita, kupumzika.

218

Magharibi

Jioni.

Amekwajuka

Amechakaa.

219

Gharighari la mauti

Karibu na kukata roho.

Siti

Mwanamke.

221

Mtima

Moyo, nadhiri au fikra ya ndani.

222

Tumai

Tumaini.

224

Wampapia

Unapiga.

227

Asikari

Askari.

228

Chepechepe

Dhaifu.

230

Azima

Kusudio, dhamira, nia.

233

Msasi

Mwindaji.

Podo

Kifuko cha kubebea mishale.

237

Nasabaye

Ukoo wake.

239

Karine

Kame.

241

Heba

Haiba, heshima na utukufu.

242

Wororo

Hali ya kuwa laini.

Mbaro

Kifungo.

244

Mziwanda

Kitmdamimba, mtoto wa mwisho.

246

Kakara

Kukurukakara, mapambano.

247

Alihozi

Alihodhi, alimiliki.

249

Iitilwe

Inaitwa.

Iwambilwe

Imewambwa.

251

Goma

Ngoma kubwa.

253

Wakifu

Takatifu.

257

Mtunzi

Mtunzaji.

258

Masikiyo

Masikio.

260

Majilisi

Baraza.

Wasiasi

Hawakuasi, walitii.

265

Inavyosinyaa

Inavyonyong'onyea, inavyopungua.

267

Mtanza

Mtaanza.

Kuteta

Kuzozana, kugombana.

272

Ukakasi

Kutumia nguvu, kulazimisha jambo.

276

Msasa

Laini.

277

Kumusia

Kumuusia.

279

Kamwagizila

Kamwagizia.

289

Lukuki

Wengisana.

292

Akahaha

Akahangaika.

Asiridhi

Asiridhike.

294

Wenzo

Wenzio.

297

Budi sina

Sina budi.

298

Tasihili

Haraka.

300

Jamala

Fadhila, matendo mazuri.

304

Tukiamiri

Tukiongoza.

306

Masurufu

Chakula cha safari.

309

Kuwajuza

Kuwapa habari, kuwafahamisha.

312

Dazani

Kumi na mbili.

Kani

Nguvu.

313

Pamwe

Pamoja.

314

Kiza kiliposhitadi

Kiza kiliposhtadi, giza lilipokoza, liliposhika sana.

315

Nyatunyatu

Kunyaria.

316

Milumba

Mbugu, nguo za magamba ya miti.

320

Nguu

Milima.

321

Ngisi

Aina ya samaki mweupe.

323

Pamba

Chakula cha safari.

325

Udhia

Tabu, usumbufu.

326

Ikawakeketa

Ikawauma.

327

Wanazivinjari

Wanazitembelea, wanazizunguka.

331

Jikusuru

Jihimu, jitahidi.

332

Kabarizi

Kazungumza.

Uchizi

Utukutu, upuuzi.

333

Kujinusuru

Kujiponya.

334

Itajulika

Itajulikana.

335

Litangia

Litaingia.

338

Konde

Shamba.

339

Wakona

Wakaona.

Azizi

Zuri.

345

Woto

Uoto, mazao.

347

Limemuumuka

Limemvimba.

348

Kudhukuru

Kueleza, kusema.

Mashukuru

Shukrani.

350

Garasha

Kitu cha ovyo kisicho na thamani.

352

Futa

Vuta.

353

Kitala

Vita.

361

Kitanga

Chombo cha udongo.

365

Iliyowasakamia

Diyowaandama.

369

Maridhawa

Vingi.

372

Usasini

Katika uwindaji.

375

Ndumba

Hirizi.

378

Walikozukia

Walipotokea.

383

Nyayu

Nyau, paka.

Halitaka

Hali takataka, hali uchafu.

386

Amiri

Mkuu, kiongozi

388

Sichi

Sichelei, siogopi.

390

Ghaidi

Jambazi.

398

Janadume

Kijana mkakamavu.

Mana

Maana.

399

Ukibalehe

Ukikomaa.

404

Kuutiringa

Kuurusha kasi.

Kumtindanga

Kumchinja.

405

Ugwe

Kamba ya upinde.

407

Tambo litajitambua

Fumbo litajifumbua.

408

Wakakirihi

Wakakinai.

410

Hari

Joto.

416

Walipojia

Walipokula chakula cha jioni.

419

Wakenda

Wakaenda.

420

Kamkabizi

Kamkabidhi.

421

Katukatu

Hata kidogo.

422

Miadini

Mahali pa kukutana.

425

Wahedi

Wa kwanza.

434

Wakamba

Wakasema.

Wa chaleni

Wa chanjo.

437

Tangua

Vunja.

440

Wakajizatiti

Wakajiandaa.

443

Suhubia

Fanyiana urafiki.

450

Nadhari

Uangalifu.

Kuzisasi

Kuzipeleleza.

452

Tamthili

Mfano wa.

453

Nyatunyatu

Tahadhari, nyatia.

Matumatu

Ghafla.

459

Akajitoma

Akajirusha.

462

Nduli

Dude, mnyama mkali.

Kibahaululi

Kijitu, kiumbe duni.

468

Bwabwa

Sauti za mbwa.

469

Rabusha

Rabsha.

470

Ananyapa

Ananyatia.

473

Usipombeze

Usitingishe.

476

Wakabwagika

Wakaanguka chini kama mzigo.

477

Yakangia

Yakaingia.

480

Lege

Legelege, mlegevu, dhaifu.

487

Nderemo

Vifijo, furaha kubwa.

489

Ahueni

Nafuu.

492

Ng'ombemwitu

Mbogo, nyati.

496

Tuu

Tu.

498

Halahala

Haraka haraka.

503

Anadhukuru

Anakumbuka.

508

Furifuri

Kwa wingi.

521

Kufura

Kufurika.

524

Nikakamke

Niwe mkakamavu.

532

Kuikita

Kuisimamisha.

535

Sahiba

Rafiki mkubwa.

537

Kaumu

Umma wa watu.

549

Nadhiri

Ahadi.

560

Twishi

Tuishi.

566

Majikalifu

Bila kutaka.

575

Miba

Miiba.

576

Alifajiri

Alfajiri.

584

Kuiegeza

Kuigesha.

586

Kuziratibu

Kuzishika (zamu).

587

Jia kijio

Kula chakula cha jioni.

Malalio

Virago vya kulalia.

589

Ja

Karpa.

Wameipambaja

Wameikumbatia.

592

Wakaishua

Wakaitia, wakaiteremsha.

595

Kafara

Sadakakwa Mizimu.

596

Kusi

Kusini.

599

Uliokoza

Wenye mwanga mkali.

622

Subalherini

Salimio la asubuhi.

624

Halahala

Himahima haraka.

627

Kwelemea

Kwenda, kuelekea.

634

Jalali

Mtukufu.

Fadhili

Hisani, msaada.

638

Kongoni

Aina ya mnyama kama nyumbu.

Kuro

Mnyama wa porini afananaye na ndama.

644

Fadhilazo

Hisani yako, msaada wako.


Mwadhamu

Mtukufu.


Masitakimu

Maslakimu, makazi.

651

Kuiauni

Kuilinda, kuitetea.

656

Wapepezi

Watu wanaowapepea watawala kwa vipepeo ili wasisumbuliwe na joto au wadudu warukao.

Wakanzi

Wakandaji.

660

Kukera

Kusumbua.

669

Nyang'au

Nduli, madude.

670

Nemsi

Ustawi.

682

Dia

Malipo mema, fidia.

690

Shahamu

Mafuta.

Dawamu

Bila kukoma, milele.

691

Mizungu

Maajabu.

693

Bahau

Mpumbavu.

694

Gomashinda

Gomatupu.

704

Saburi

Subira.

708

Wafane

Waliofana, wema, wazuri.

714

Hirimu

Kundi la umri fulani.

Rika

Watu wa uniri fulani.

716

Mifuo

Mitaro iliyochimbwa na maji.

717

Ukufi

Kitu kidogo.

719

Wakajitoma sharini

Wakajitosa katika pilikapilika.

720

Vitimbi

Hila, ujanja.

728

Hio

Hiyo.

733

Janga

Balaa, maafa.

735

Kauri

Chombo cha udongo.

740

Kawashua

Kawadharau, kuwashushia hadhi.

742

Amali

Matendo.

743

Ikacharuka

Ikalipuka.

746

Nti

Nchi, ardhi.

747

Kutowelea

Kufanya kitoweo.

752

Ikaputa

Ikavimba kama puto.

754

Furusa

Fursa, nafasi.

763

Kaumu

Umma wa watu.

764

Walitafakari

Waliwaza kwa makini.

768

Harara

Haraka.

772

Ziwazingile

Ziliwazunguka.

773

Juku

Jukumu.

776

Wasioneke

Wasionekane.

782

Ametarama

Amestarehe.

783

Vikuku

Mabangili,

785

Bwabwaja

Porojo.

788

Adhamu

Hadhi, heshima.

789

Maajuza

Wakongwe.

791

Kujalisi

Kuongea, kujadiliana.

795

Dubwana

Dude, nduli.

Hiana

Uhaini, uadui.

798

Kukuambua

Kukunyanganya.

803

Ndwele

Maradhs, ugonjwa.

804

Mtufala

Mtu duni, mjinga.

805

Nadhari

Akili, uangalifu.

808

Maki

Kina.

825

Havaa

Nilivaa.

828

Nimekufuru

Nimetenda mambo yenye kuwachukiza Miungu.

829

Kujisoza

Kujiumiza.

834

Dhalimu

Anayedhulumu.

835

Aliyoiatamia

Aliyoimilild.

850

Nyumao

Nyuma yao.

853

Dhuluma

Uonevu.

856

Misu

Majisu makubwa.

859

Madhila

Maafa.

862

Bimbirishana

Angushana.

873

Sahibu

Rafiki.