
| Utenzi wa Nyakiiru Kibi (ECOL Publications, 1997, 109 p.) |
|

Taswira
1
Leo nimekusudia
Hadithi kusimulia
Kutoka
hisitoria
Ya nchi ya Tanzania.
2
Ni hadithi ya zamani
Ni hadithi ya thamani
Ni mambo
yetu ya ndani
Mababu walitwachia.
3
Nimepewa na wahenga
Ndipo nami
nikapanga
Halafu nikayatunga
Na nyinyi kuwapada.
4
Ndipo leo nathubutu
Habari za babu zetu
Za kale ya
nchi yetu
Vijana kuwaambia.
5
Nianze kuhadithia
Mambo yalivyotukia
Ili mpate
sikia
Na pia kuzingatia.
6
Ni simulizi za kale
Za wahenga na
wavyele
Waloishi enzi zile
Ambazo zimepotea.
7
Ambazo zimepotea
Pasina na kurejea
Mageni
yamefagia
Ya jadi yamefukia.
8
Basi na twende Bukoba
Ufalume wa Kiziba
Nchi
ya nyingi rutuba
Na ardhi inayozaa.
9
Zamani yafikirika
Mwaka elufu hakika
Na mia
nne kuweka
Ndipo yalipotukia.
10
Enzi hizo za zamani
Kiziba masikanini
Wahenga
walisakini
Wakila na kujinywea.
11
Watu hao wa zamani
Walikuwa na imani
Na mila na zao
dini
Zikiwaonyesha njia.
12
Wali na Miungu wao
Tofauti na wa
leo
Na Mizimu wenye vyeo
Na Mahoka asilia.
13
Walimjua Ruhanga
Muumba nchi na
anga
Na kila kinachotanga
Katika hii dunia.
14
Bwana wa tangu na tangu
Asili ya ullmwengu
Mshika
tamu na chungu
Mtawala wa dunia.
15
Mungu aliyetukuka
Mungu wa Waafirika
Ambaye
hakuumbika
Na hawezi kwangamia.
16
Aishiye Kuzimuni
Na kuona ya nchini
Na
kusambaza auni
Kwa wanaohitajia.
17
Hayupo wa kumzidi
Wala wa kumkaidi
Sauti yake ni
radi
Na jicho lake ni jua.

Taswira
18
Huona yalofichika
Hushika yasoshikika
Hujua
yasojulika
Atoaye na kutwaa.
19
Hako katika majengo
Ya minara na maringo
Na
paa zenye migongo
Watu wanayoinua.
20
Hakuhitaji wajumbe
Wa kutuma kwa viumbe
Kwake hapana
wapambe
Wote ni sawa sawia.
21
Hakuhitaji mitume
Kwa wake na wanaume
Manabii wenye
tume
Pia hakuwatumia.
22
Hakuwa na misahafu
Kwelezawe utukufu
Kurasa
vitu dhaifu
Katu hakuvitumia.
23
Misahafuye Umbile
Na vyote vilivyo mle
Milima
yenye vilele
Nyota, sayari na jua.
24
Yumo katika miamba
Na maziwa yenye mamba
Na moyoni
mwa mgomba
Malikia wa mimea.
25
Vema utamsikia
Katika radi ya mvua
Ngurumo,
tufani pia
Vyote alivyoumbia.

Taswira
26
Hana mke hana mwana
Na ndugu wa kuzawana
Yu
baba, ndugu na bwana
Kwa watu wote sawia.
27
Ndiye aliumba Kintu
Baba wa wahenga
wetu
Ni babu wa kila kitu
Humu katika dunia.
28
Ndiye alimpa mwenzi
Mwandani wake
Kikazi
Ili wafanye uzazi
Watu kujaza dunia.
29
Kikazi yu mwanamke
Kintu kawa mume wake
Na dunia ili
pweke
Bila mtu kulowea.
30
Ruhanga hakuwa pweke
Ali na Miungu wake
Waume
na wanawake
Wakiongoza dunia.
31
Alikuwepo Mugasha
Mungu wa Ziwa
Mtisha
Tufani anafurusha
Piaupepo namvua.
32
Na huyu katanda hasa
Kwa Wasukuma ni
Ngassa
Kwa Waganda ni Mukasa
Hata Rwanda yuko
pia.
33
Naye Muungu mjanja
Ana mguu mmoja
Huishi katika
nyanja
Lweru ndo Vikitoria.
34
Mtawala wa ngurumo
Umemena mtetemo
Maziwa na
vilivyomo
Bahari, tufani, mvua.
35
Pia bibi Nyakalembe
Wa kilimo na
majembe
Mke wa Mugasha kumbe
Mashamba asimamia.
36
Alikuwepo Kasana
Mungu wa wawinda
sana
Na aridhi ni dhamana
Yote kaishikilia.
37
Alikuwepo Irungu
Mwenye uta na
kirungu
Mapori ya ulimwengu
Yote amejitwalia.
38
Alikuwepo Lyangombe
Bwana wa wachunga
ng'ombe
Hutawala kila pembe
Ng'ombe wanapofugiwa.
39
Yupo Kaihura-Nkuba
Mungu-Radi na
dhoruba
Mugasha ni wake baba
Nyayo anafuada.
40
Alikuwepo Wamala
Wachwezi
awatawala
Yote ndiye huyamala
Watu yakiwazidia.
41
Pia Kagoro mahiri
Naye Muchwezi
jasiri
Babaye alomkiri
Ni Wamala nakwambia.
42
Yupo Kilo siyo chuku
Ni Muungu wa
usiku
Penye kiza humpiku
Huona bila ya taa.
43
Yupo naye Bibi Kasi
Kilimoni ndiye
bosi
Na Bi Rugila ni nesi
Uzazi ndiye hutoa.
44
Nao wengine Mahoka
Wachwezi walotukuka
Japo
sikuwaandika
Walihimidiwa pia.
45
Kwisha wataja Wachwezi
Watukufu wenye
ezi
Ndipo naianza kazi
Ya wimbo kuwaimbia.
46
Ya utungo kutongoa
Kwa vina kupangilia
Na
kunga kufuatia
Kwa mahadhi ya halua.
47
Ni mengi ya kuhadithi
Ya wema na
uhabithi
Ya uzazi na urithi
Na ya urafiki pia.
48
Yote kwa ukamilifu
Pia kwa uaminifu
Kwa ufupi na
urefu
Nataka kusimulia.
49
Mshike wana wa leo
Nao watoto wajao
Mjue taifa
ndio
Hapo lilikoanzia.
50
Mjue zamani hizo
Kulivyokuwa mzozo
Matetano
mzomzo
Kwa tumbo kupigania.
51
Mjue pia hakika
Mambo yaliyotukuka
Mazuri ya
kupendeka
Mwanzo yaliyotukia.
52
Halafu kale mpishe
Ya leo mlinganishe
Muone kama
kasheshe
Zingali zaendelea.
53
Sasa turudi Kiziba
Kwenye nchi ya rufuba
Na waume
wa miraba
Na wake wenye kuzaa.
54
Nchi njema ya kuwanda
Ya uzuri wa
kutanda
Milima mingi na nyanda
Zenye rutuha murua.
55
Huko zama za zamani
Mwa ziwa ujiranini
Aliishi
sulutani
Mkali kupindukia.
56
Jina lake mwenye ezi
Takwambia waziwazi
Ujue na
kumaizi
Ni Ntumwa ninakwambia.
57
Na huyu Ntumwa hakika
Uzinzani alitoka
Kiziba
alipofika
Nchi akajitwalia.
58
Alimuua maliki
Kwa kumpiga mkuki
Akachukua
miliki
Na watu kuwaonea.
59
Alomwua jina lake
Akitwa Mukama
Bike
Mukama wadhifa wake
Ni Mfalume sikia
60
Kaingia kwa mabavu
Akatawala kwanguvu
Kwa kazi ali
mvivu
Bali siyo kwa kuua!
61
Kunyonga alikujua
Kukata mashingo pia
Kunyonya na
kukamua
Pia alipendelea.
62
Alitawala Kiziba
Ndiyo nchi ya Waziba
Wazaao na
kubeba
Kwa wingi wa kuzidia.
63
Yali na majimbo mengi
Nchi hii yenye
vingi
Kanyigo ndiko msingi
Mukama alikokaa.
64
Mengine Ishozi, Gera
Kayanga, Bwanja na
Bwera
Buyango kwa masogora
Na Ruzinga kuishia.
65
Na vijiji vya mpaka
Lukurungo,
Bugandika
Katendagulo, Kashaka
Bukoba waelekea.
66
Haya yote ni majimbo
Yenye waume wa
tambo
Kanyigo ndicho kiambo
Mukama alipokaa.
67
Kijiji ni Kigarama
Alipoishi Mukama
Kwa ubwana na
heshima
Akila na kujinywea.
68
Na kutoka Kigarama
Waona ziwa
lahema
Kaskazi kitazama
Buganda waangalia.

Taswira
69
Na mukama kwenye nyumba
Alikula akavimba
Kitambi
kikamyumba
Na mashavu kuzidia.
70
Kwa kufuma na kuuma
Kwa husuma na
hujuma
Bilahuruma Mukama
Mali akijitwalia.
71
Akiona mwanamke
Mwenye uzuri wa peke
Humuua mume
wake
Mke akajitwalia.
72
Watu 'kiwatia ngwamba
Na inazao
akisomba
Akinyang'anya mashamba
Ya masikini raia.
73
Na kila anayepinga
Mpumbavu hana kinga
Anakatwa kwa
upanga
Hakawizwi nakwambia.

Taswira
74
Basi hata siku moja
Mkewe mzito mja
Alijaliwa
faraja
Mtoto kujifungua.
75
Likapigwa la mgambo
Likilia lina jambo
Ikuluni
kuna mambo
Kajifungua malkia.
76
Malikia mtukufu
Kazaa mwana
nadhifu
Mwingine hafui dafu
Kunawiri kazidia.
77
Ikaenea habari
Kama pepo za bahari
Malikia wa
fahari
Leo amejifungua!
78
Pigeni nanga nazeze
Pigeni ngoma
mcheze
Marimba yakerereze
Mrithi ametokea!

Taswira

Taswira

Taswira
79
Unajuaje: Huenda
Mwana mema akatenda
Na haki
akazilinda
Kiti akikikalia.
80
Huenda akawa mwamba
Shujaa mwenye
kutamba
Kiziba akaipamba
Sifaze zikatangaa!
81
Kwa hamu na kwa shauku
Wananchi
pukupuku
Kutoka huko na huku
Wakaja kushuhudia.

Taswira
82
Wakaja kumsalimu
Maliki aso makamu
Ambaye
hajafahamu
Kuwa hii ni dunia.
83
Na magoma yakatika
Na nanga zikanangika
Na watu
wakachemka
Kwa furaha kuzidia.
84
Ntumwa akaarifiwa
Mtoto keshazaliwa
Akenda kwa
tuwatuwa
Mwanawe kuangalia.
85
Kwa taabu ya uzito
Kenda kwa mjikokoto
Akikita
batobato
Nyayo zake kwenye njia
86
Akafika akaona
Mkewe na pia mwana
Kipara
akajikuna
Kwa mawazo kumjaa.
87
Akarejea nyumbani
Kufikiri kwa makini
Lipi
linayumkini
Mtoto kumtendea.
88
Hapo kaitwa mganga
Ampe mtoto kinga
Asije patwa na
janga
Mikasa ya kumuua.
89
Na mganga asisite
Akaleta dawa
zote
Ngisha mitishamba yote
Mwana ya kumkingia.
90
Mwana awe na afia
Asikumbane na
waa
Na awe mtu shujaa
Kitu asiyechelea.

Taswira
91
Akue ahodhi shamba
Akomae awe
baba
Ahodhi ng'ombe si haba
Na maziwa kujinywea.
92
Shambale lirutubike
Ndizi
zisilitindike
Mali iwe mwenzi wake
Ashike na kuachia.
93
Apate wake aoe
Watoto wamzalie
Heshima
imfikie
Fahari na nguvu pia.
94
Baada ya hayo kuwa
Mtoto aliachiwa
Kwa mamaye
kulelewa
Maziwa kujinyonyea.
95
Siku zikapanda ngazi
Majuma yakawa
myezi
Ikaonekana wazi
Mwana meno yatamea.
96
Tayari meno ya kwanza
Yataka
kujitokeza
Katonda twamtukuza
Mizimu, wahenga
pia!
97
Mama akafurahika
Atukuzwe Mtukuka
Mwana wangu
mpendeka
Meno atajiotea.
98
Mafizi yamekomaa
Sikuze
zakaribia
Zakaribianajua
Mwana nilijizalia.
99
Na yule Ntumwa Mukaina
Hana raha anahema
Mawazoye
siyo mema
Kwa mwana aliyezaa.
100
Huyu mwana anidsha
Anitisha vya kutosha
Bado
ninayo maisha
Mrithi sijawania.
101
Bado kijana kabisa
Tena mtu wa kisasa
Sitaki
wanasiasa
Mambo kuyaingilia.
102
Nani anayeelewa
Labuda akisha
kuwa
Atadai kuchukuwa
Kiti nilichokalia?
103
Afadhali kuzuia
Ugonjwa haujakua
Kuliko
kuungojea
Hadi unapozidia.
104
Hadhari kwa mtawala
Ni jambo liso
na dhila
Wangapi wafanya hila
Ukama kuunyakua?
105
Wangapi wanichekea
Sifa
wakinipalia
Ambao wangependea
Kiti changu kukalia?
106
Wangapi wangetamani
Kutwaa usulutani
Mali
zangu za thamani
Namashamba kuchukua?
107
Wangapi rafiki zangu
Watamani kwa
uchungu
Kulia chunguni mwangu
Nyama zangu kubugia?
108
Moyo wa kibinadamu
Nami
ninaufahamu
Nimeshashika hatamu
Kamwe sitaiachia!
109
Ninaelewa hakika
Katu
sitadanganyika
Nimekwisha kunyanyuka
Chini sitakurejea.
110
Mimi bado ni kijana
Bado nitazaa wana
Sasa
hivi ni laana
Vifaranga kutotoa!
111
Na papo hapo Mukama
Kwa amri akatuma
Mganga aitwe
hima
Analo la kumwambia.
112
Mganga kupata wito
Akazikoroga kwato
Macho
yamuwaka moto
Kwa furaha kuzidia.
113
Kufika akasalimu
Mukama kumheshimu
Kwa adabu na kwa
hamu
Kama ilivyo sheria.
114
Na Ntumwa akamwambia
Mganga nimesikia
U
mahiri kuzidia
Kila kitu unajua.
115
Sasa mimi nina haja
Ambayo nitaitaja
Ndipo
hakuita kuja
Mbele zangu kukwambia.
116
Kabula sijaisema
Nataka ahadi
hima
Hapa uliposimama
Ya kuwa hutakataa.
117
Niambie: Uko radhi
Haja yangu
kuikidhi
Kwa manufaa na hadhi
Yangu na wote raia?
118
Na mganga akajibu
Bwana wajuajawabu
Mimi
kwangu ni wajibu
Mukama kutumikia.
119
Kuisha hayo kusema
Akamwambia Mukama
Mimi
sasa nitasema
Jambo nililokwitia.
120
Nataka ujitahidi
Kwaakili najuhudi
Kutumia
dawa dhidi
Adui yangu sikia.
121
Adui huyo ni toto
Zao langu la majuto
Nimeota
kwenye ndoto
Litaja kunivamia.
122
Jitoto hilo ni moto
Ni moto wa
mtokoto
Kulizaa sina pato
Ila nikuteketea!
123
Sasa muda umepita
Meno yatanza kuota
Kayazuie
kuota
Uachie ya balaa.
124
Kwa uwezo wako wote
Na kwa dawa zako
zote
Hili dmiza upate
Nchi kuniokolea.
125
Na uende ukijua
Thawabu
yakungojea
Mengi nitakupatia
Hiliukinifanyia.
126
Mganga akaitika
E walla, E Mtukuka
Yote
yatatimilika
Unayoyahitajia.
127
Kwisha hayo akatoka
Karejea kwa haraka
Na nyumbani
akafika
Dawa akajitwalia.
128
Kisha hapo tasihili
Na tunguri zake
mbili
Ndani ya kapu la kili
Kaenda kwa Malikia.
129
Kwenye ya mshonge nyumba
Ilozungukwa
migomba
Akafika akaomba
Ruhusa akaingia.
130
Kaingia na kuona
Mzazi na wake mwana
Chipukizi nalo
shina
Sebuleni wamekaa.
131
Kasabahi kamaliza
Na kisha
akaeleza
Nimetumwa kufanyiza
Dawa zangu za afua.
132
Kanagiza kwa makini
Simba wa humu
nchini
Fizi za mwana yakini
Nije kuzinuizia.
133
Akomae fizi zake
Anawiri kanwa
kake
Azungumze acheke
Na matoke kujilia.
134
Maharage bila wasi
Napia nyama
yabisi
Aweze kula upesi
Na ladha kufurahia.
135
Malkia akaeleza
Bwanangu
namtukuza
Fanyiza unayoweza
Mwanameno kupada.

Taswira
136
Na muda huo kichanga
Chatabasamu kijinga
Kakitoa
kwa mganga
Mganga kakipokea.
137
Kishapo akachukuwa
Aina nyingi za dawa
Sisi
tusiozijuwa
Mwenyewe azitambua.
138
Kafunua kanwa kake
Yule mwana wa
makeke
Kisha hizo dawa zake
Moja moja kamtia.
139
Hii dawa ya kukaga
Wachawi
wanaologa
Fizi za wana wachanga,
Kinywani akamda.
140
Hii dawa ya kunoa
Meno yapate toboa
Mafizi na
kutokea,
Kinywani akamtia.
141
Hii ya kulainisha
Mafizi
kudhalilisha
Meno yapate pitisha,
Kinywani akamtia

Taswira
142
Hii ni ya kutobanga
Mipango
wanayopanga
Maadui wa kichanga,
Kinywani akamda.
143
Kamaliza kumtia
Madawa hayo mamia
Maneno
kunuizia
Na kisha kumsugua.
144
Kamsugua ugino
Kwa ari iso
kifano
Ili ukaote meno
Meno ya kutafunia.
145
Bali kwa siri mganga
Wajuu tu kauganga
Naye mama wa
kichanga
Hili hakulitambua.
146
Fizi la juu 'kafanza
Hata akalibonyeza
La
chini akalisaza
Hakulishughulikia.
147
Kua, mwana wangu, kuwa
Kua upate
mabawa
Ukaruke kama njiwa
Na mawinguni kupaa.
148
Kua na uwe shujaa
Adui upate ua
Nchi ipate
kujua
Na jinalo kutangaa.
149
Nakupa yangu baraka
Sudi njema
nakuvika
Kua upate lukuka
Katika hii dunia.
150
Kamganga kamaliza
Mtoto
kamuengeza
Siku kadha utaweza
Nyama kuishambulia.
151
Kumsifia akisha
Mikono kajipangusha
Tunguri
kazifungasha
Kaaga kajiendea.
152
Katoka ajipongeza
Hakika nimemuweza
Mukama
atanitunza
Mengi atanipatia.
153
Na siku chache kupita
Mambo yakawa matata
Mwana
meno amepata
Bali hofu yanada.
154
Meno yanada hofu
Meno yana uhalifu
Meno yanaleta
ufu
Kwa Bwana na Malikia!
155
Meno yanaleta dhiki
Meno yatazua chuki
Meno yaleta
mikiki
Ya misiba na balaa!
156
Tazama mkasa huu
Kaota meno yajuu!
Kweli haya
ni makuu:
Ni alama ya balaa!
157
Meno nani kasikia
Ya juu kutangulia
Ya chini
hayajangia
Fizini kujitokeza!
158
Twamhofia Mukama
Ufalumewe mzima
Katu
hautasimama
Haya yakiendelea!
159
Naye yule Malikia
Kuona yalotokea
Akalia,
akalia
Mwanangu wamemuua!
160
Wameniulia mwana
Kwa kumda laana
Ni
heri kuwa kitwana
Kuliko haya kwambua.
161
Heri kuwa kijakazi
Kuishi kwenye
masizi
Kuliko kuwa mzazi
Wa mwana mwenye balaa.
162
Heri mimi kwangamia
Kuliko
kutokomea
Kwa sababu ya balaa
Mwana niliyemzaa!
163
Na alaumiwe yule
Aliyethubutu vile
kuleta
ulozi ule
Mwanangu kumpalia.
164
E Mugasha mwenye kafi
Mchawi mpige
kofi
Aishi maisha ghafi
Afe bado apumua!
165
Na habari ikatanda
Ikatanda na
kuranda
Ikaranda na kuwanda
Nchi yote kuenea.
166
Na magoma yakadunda
Mithili ya debe
shinda
Zikapulizwa na panda
Maafa yametokea.
167
Maafa yametokea
Kuichafua dunia
Mtoto wa
Malikia
Ndiye mletaji baa!
168
Zikafika sikioni
Mwake Ntumwa
kasirini
Akaelewa moyoni
Mganga amepatia.
169
Wakafika vijakazi
Huku walia machozi
Mbele ya kiti
cha ezi
Msiba kuutongoa.
170
Mukama akisikia
Ainri akaitoa
Wajakazi
kuwaua
Wamemtia fadhaa!
171
Wazana wakauawa
Viungo
kukongolewa
Na kuachiwa kengewa
Miambani kujilia.

Taswira
172
Na Ntumwa akasimama
Alia na kulalama
E
Ruhanga! Mungu mwema
Kwa nini kunionea?
173
Oh! Nisiye na bahati!
Oh! Ningekuwa
maiti!
Waseme Ntumwa hayati
Kuliko hiki kuzaa!
174
Wakasikia raia
Mukama akiugua
Huruma
wakamwonea
Kwa yaliyomwangukia.
175
Na wakafika harara
Wazee wenye
vipara
Bami walio na ghera
Ya nchi kuiokoa.
176
Wajuao kila mila
Kila ada, kila hila
Wajuzi
wenye jamala
Na heshima kwa raia.
177
Kwa majonzi wakafika
Machozi yawadondoka
Miguuni pa
malika
Wote wakasujudia.

Taswira
178
Wakasujudu: Hdbuka
Ewe
Simba mtukuka
E! Lugaba msikika
Tunakuomba sikia.
179
Sikiza Mukama wetu
Wasemayo wako watu
Wazee
wa nchi yetu
Walezi wa jumuia.
180
Nchi imeangukiwa
Na balaa bila dawa
Miliki
yanajisiwa
Na nafusi yako pia.
181
Sisi pia tu wazazi
Tuna wana na
wakazi
Hivyo twalia machozi
Haya tunapokwambia.
182
Majonzi yametukaba
Twasakamwa na msiba
Bali
mila za mababa
Hatuwezi kwingilia.
183
Kuingilia ni shari
Mizimu
watakasiri
Nchi wataihasiri
Na watu kuangamia.
184
Hivyo baba tunasihi
Twasihi wako
wajihi
Kiri leo asubuhi
Mila yetu kutimia.
185
Akasema mfalume
Pulikeni
wanaume
Timizeni hiyo tume
Ya Mizimu wa afua.
186
Jambo limesha tukia
Baa limetupitia
Pigo
limetwangukia
Ni bure kulizuia.
187
Naugulia uzazi
Naugulia
ulezi
Vijaluba vya machozi
Vyataka kujifumua!
188
Hata sasa hali sina
Macho
yanisinasina
Ningelia kama mwana
Lakini najizuia.
189
Ningetamani kulia
Bali ninajizuia
Sulutani
akilia
Miliki huangamia!
190
Wakisikia majaji
Bwana wakamfariji
Kishapo mbele ya
taji
Wakajiondokelea.
191
Wakatoka wakaenda
Mioyo inawadunda
Cha malikia
kibanda
Wakabisha na kungia.
192
Wakasema: Leta mwana
Tena kwa haraka
sana
Leta mwana wa laana
Tupate kumchukua!
193
Akabisha Malikia
Mwana hamtachukua
Kabula ya
kuniua
Hapa nilipokalia!
194
Wakasema: Hilo mwiko
Sisi tu raia
zako
Twataka tunutu lako
Si roho ya Malikia!
195
Malikia akalia
Machozi kumlowea
Sikubali
nawambia
Mwanangu kunitwalia!
196
Mnataka kuniziba
Raha tamu ya kubeba
Na
kumlea kwa huba
Mwana niliyemzaa.
197
Furaha ya kuliwaza
Raha ya kubembeleza
Mtoto
anapocheza
Mwaja kunizuilia.
198
Wa heri mama wagumba
Wasiofahamu mimba
Mateso
ya myezi saba
Na miwili kwongezea.
199
Wasiojua ajizi
Na mateso ya
ukazi
Na uchungu wa uzazi
Na taabu za kulea.
200
Heri kutozaa tena
Heri umama kukana
Kuliko
kuzaa mwana
Usimwone anakua.
201
Sikuzaa nimzike
Mwana wangu wa upweke
Bali
yeye anizike
Siku itapowadia.
202
Mzazi kuzika mwana
Ni kipeo cha
midhana
Nani tadumisha jina
Lake katika dunia?
203
Nani takuza ukoo
Kwa kuongeza uzao
Nani
tatunza mizio
Na mila za jumuia?
204
Mwanondolea mwangaza
Kwa mwanangu
kupoteza
Sasa usoni ni kiza
Maisha yamenishia!
205
Akalia, akalia
Anga akalipasua
Moyo
ukamuugua
Akalia Malikia!

Taswira
206
Wazee wale kwa nguvu
Na kwa mioyo mikavu
Kitoto
chenye utuvu
Mama wakamtwalia.
207
Mama kuleta matata
Wakamfunga kakata
Na
kumuacha aguta
Alia na kuugua.
208
Nasikuchache kupita
Mauti yakamuita
Roho yake
akakata
Kamba akaiachia!
209
Wazee wakasafiri
Nacho kitoto kizuri
Siku moja ya
safari
Mpakani wakatua.
210
Wakatua mpakani
Na kwingia mashuani
Kuvuka hadi
ng'amboni
Kibumbiro kuingia.
211
Kagera wakauvuka
Na Kitara wakafika
Mila
iliyotukuka
Wapate kutimizia.

Taswira
212
Na Kibumbiro wakaja
Nchi ya mti mmoja
Nchi ya vingi
vioja
Nchi ya kiu na njaa.
213
Ukingoni mwaKagera
Penye viboko na vyura
Mtoto
wakamgura
Kanyigo wakarejea.
214
Wakamuacha mtoto
Alia bila msito
Shingoni
hirizi nzito
Ya ukoo kavalia.
215
Na mtoto akabaki
Analia hasikiki
Amezungukwa na
dhiki
Navitisho vyadunia.
216
Viboko wananguruma
Vifaru wanakoroma
Mamba
wanahemahema
Yeye amejilalia!
217
Hoi kwa njaa na kiu
Kando ya mto mkuu
Macho
kayakaza juu
Chali amejilalia.

Taswira
218
Magharibi ikafika
Mtoto
amekwajuka
Koo limemkauka
Sauti imepwelea.
219
Gharighari la mauti
Akapita mwana
siti
Yo! Hapakunamaiti!'
Akataka kukimbia.
220
Kuni zikamponyoka
Ambazo amezishika
Yowe
likamdondoka
Roho ikamkimbia!

Taswira
221
Bali mtima wa pili
Ukamtia akili
Kwani
kukimbia hili
Nini unachohofia?
222
Na hata kama ukifa
Huna hasara kwa kufa
Huna
tumai la sifa
Wala kuwa Malikia.
223
Wacha uwoga uende
Udadisi umpande
Akapiga moyo
konde
Mtoto akamwendea!
224
Kumfikia kaona
Bado yu mzima mwana
Bado macho
yanaona
Na moyo wampapia.
225
Akamwinua kwa wema
Mtoto moto kwa homa
Mzuri
kama Mukama
Huyu mwana angalia!
226
Atakuwa mwana wangu
Katika uzee
wangu
Nitamchukua kwangu
Upweke tanondolea.
227
Nitamlea vizuri
Nitamfunza ya heri
Atakuwa
asikari
Muda atakapokua.
228
Kichwa kikiwa cheupe
Na maungo
chepechepe
Moyo utawa mweupe
Furaha tanipatia.
229
Kampeleka nyumbani
Kwa shangwe iso kifani
Wakafika
majirani
Mwana kumuangalia.
230
Baraza likaitishwa
Azima
ikapitishwa
Aitwe Kanyamaishwa
Mwana wa nyika sikia.
231
Yu mtoto wa porini
Kwani kakutwa mwituni
Jina hilo
silo duni
Ukweli laelezea.
232
Na mtoto akaishi
Bila mwingi ushawishi
Akawa mtu wa
jeshi
Kijana wa ushujaa.
233
Pia akawa muwinda
Msasi katika nyanda
Upinde
akaupinda
Podo akajisukia.
234
Na ukipita wakati
Bibi kapatwa mauti
Kama wengine
hayati
Waliomtangulia.
235
Kanyamaishwa kalia
Kaburini kamtia
Matanga
kamkalia
Kama ilivyo tabia.
236
Kwa upweke akabaki
Mwisho kaona ni dhiki
Katafuta
mshiriki
Mke akajiolea.
237
Walakini hakujua
Wapi alikotokea
Nasabaye
asilia
Katu
hakuitambua.