Cover Image
close this bookFasihi, Uandishi na Uchapishaji (Dar Es Salaam University Press, 1993, 260 p.)
close this folderSEHEMU YA KWANZA: UWAVITA
View the document1. Historia na Maendeleo ya Umoja wa Waandishi Vitabu Tanzania (UWAVITA)
View the document2. Maaumio ya Washiriki wa Semina ya Kitaifa ya Waandishi na Wahakiki wa Vitabu Iliyofanyika Dar es Salaam 26 - 29 Octoba, 1987

1. Historia na Maendeleo ya Umoja wa Waandishi Vitabu Tanzania (UWAVITA)

I.C. Mbenna

1. Vyama vya waandishi sio wazo geni katika nchi yetu. Hata wakati wa ukoloni vijana shuleni waliunda au walishawishiwa na waliniu wao kuunda vikundi vya waandishi wa gazeti la shule, michezo ya kuigiza, vichekesho, mashairi na kadhalika. Tofauti iliyopo ni kwamba hawakuhimizwa kuendelea na vikundi hivyo baada ya kumaliza masomo yao. Zaidi ya hayo, mawazo yaliyopendelewa zaidi ni yale ya kutukuza ukoloni, nadharia na starehe tu.

2. Watu wachache waliodiriki kuendelea na uandishi kwa ajili ya magazeti na vitabu, kwa mfano, Shaaban Robert, A. Abedi Kaluta na Mathias Mnyampala hawakupata tuzo linalostahili kwa kazi yao, na walikuwa mara nyingi katika hatari ya kushtakiwa au kushutumiwa na serikali ya kikoloni.

3. Miaka michache tu baada ya kupata uhuru na kuwa na serikali yetu, Watanganyika wachache waliokuwa wakiishi Dar es Salaam walijiunga na kuanzisha chama cha waandishi kikiitwa "Tanzania Writers Association." Kwa kuwa waliokuwa na uwezo wa kuandika vitabu walikuwa wachache sana, chama hiki hakikujulikana na hakikuhimili misukosuko.

4. Hata hivyo baadaye walijitokeza wananchi wengine wenye upenzi na mashairi wakaunda chama chao "UKUTA" (Usanifu wa Kiswahili na Ushairi Tanzania). Bado chama hiki kinajikokota pamoja na matatizo yake ya fedha.

5. Vuguvugu lilikuwa kubwa aidi mnamo mwaka 1974 wakati vijana wachache, wafanyakazi Dar es Salaam, walipojiunga na kuanzisha chama "WAANDISHI WA VITABU TANZANIA (WAVITA)." Kiliongozwa na Ndugu I.C. Mbenna (Mwenyeldti), Ndugu Rashid Sdf (Makamu Mwenyekiti), Jumaa Mkabarah (Katibu), J.P. Mbonde (Mwekahazina).

6. Maombi ya kuandikisha chama yalipelekwa Machi 1974 kwa Msajili wa Vyama, Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi. Wizara zinazohusika zilikaa na maombi hayo hadi 24 Februari, 1976 kilipopewa hati Na. So. 5908.

7. Mnamo mwanzoni mwa 1977 kikajitokeza kikundi kingine katika mji wa Dodoma. Kikundi hicho kilikuwa kikiongozwa na Ndugu Shemshanga. Na shabaha yake ilikuwa ileile ya kuwaunganisha waandishi wa vitabu na kuwahimiza waandike. Kikundi hicho kilijiita "UMOJA WA WAANDISHI VITABU TANZANIA (UWAVITA)"

8. Kwa bahati njema wakagundua kuwa kipo chama kingine Dar es Salaam; na kwamba si vyema kuzusha vikundi mbalimbali vyenye shabaha na lengo moja.

9. Jitihada zikafanywa kukutanisha vikundi viwili hivyo ili kuunda chombo kimoja kitaifa. Makubaliano yalipatikana na maombi ya kubadili jina na katiba yakatumwa kwa Msajili wa Vyama tarehe 23.3.1977.

10. Kabla Msajili hajakubali mabadiliko hayo, ikafahamika kuwa kuna kikundi kingine kilichokuwa kikitaka kuandildshwa tangu 1975 hadi 1978 na kilikuwa bado kupata hati. Kikundi hicho kilijiita "UMOJA WA WAANDISHI NA WAFASIRI VITABU TANZANIA (UWAVITA)." Kikundi kiliongozwa na Ndugu F.F. Kawegere na Abass Abdallah Ishabailu huko Mwadui, Shinyanga. Masjala ya vyama ikatataoishwa na kufanana kwa majina na katiba, na ikawa vigumu kuvitofautisha vikundi hivyo.

11. Kwa bahati nzuri, vikundi hivi viwili vikakubaliana, chini ya ushauri wa Msajili wa Vyama, kuungana tarehe 10.10.1978. Katiba mpya ikaandaliwa na jina likawa UMOJA WA WAANDISHI WA VITABU TANZANIA (UWAVITA) na kuandikishwa upya tarehe 17.8.1979.

12. Viongozi wa awali walikuwa:

Mwenyekiti:

Ndugu Leonard John Kawala

Makamu Mwenyekiti:

Ndugu Euphrase Kezilahabi

Katibu Mkuu:

Ndugu Irenei Cassian Mbenna

Mweka Hazina:

Ndugu Dadi Mwaware

Mlezl:

Ndugu Ibrahim Kaduma

Wadhamini:

Ndugu Ezekiel Kaungamno

Ndugu Nazareno Ngulukulu

13. Baada va kufanya marekebisho machache katika Katiba. uchaguzi wa viongozi ulifanyika tarehe 16.3.1985 na 11.4.1987. Nafasi zilizojazwa ni kama ifuatavyo:

Mwenyekiti:

Ndugu Euphrase Kezilahabi

Katibu Mkuu:

Ndugu Irenei Cassian Mbenna

Mwekahazina:

Ndugu Richard Mabala

Mhariri Mkuu:

Ndugu M.M. Mulokozi

Katibu Mwenezi:

Ndugu H.G. Mwakyembe

14. UWAVITA ni chama pekee kitaifa na matawi yanaweza kuanzishwa popote Tanzania. Matawi ya kwanza yalikuwa Dar es Salaam, Mwadui na Dodoma. Sasa yamebakia Dar es Salaam na Kigoma. Mengine yamekufa kutokana na kuhama kwa wanachama.

15. Kwa upande wa ushirikiano na vyombo vingine, UWAVITA kimewakilishwa na Katibu Mkuu, Ndugu Mbenna, katika mkutano wa kimataifa wa "Afro-Asian Writers Association " huko Urusi, Aprili 1979; na katika semina ya kimataifa ya Kiswahili iliyoendeshwa na TUKI, Chuo Kikuu cha Dar es Salaam, 1978 na 1980. Zaidi ya hayo kimetembelewa na mwandishi wa Kirusi, Komredi Nickolai A. Anastasyev na waandishi wengine wa Urusi, Uchina na Misri.

Semina ya waandishi ya tarehe 26.10.87 hadi 29.10.87 imefanyika kutokana na misaada na ushirikiano wa vyombo mbalimbali vya kitaifa na kimataifa. Watu, vyombo na mashirika hayo ni pamoja na:

(i) Baraza la Kiswahili la Taifa
(ii) Balozi Yusushi Kurokochi wa Japan
(iii) Profesa Hino wa Japan
(iv) Ubalozi wa Ujerumani Magharibi (FRG)
(v) Waandishi wa Japan
(vi) Ubalozi wa China
(vii) Ubalozi wa Norway (NORAD)
(viii) Wizara ya Maendeleo ya Jamii, Utamaduni, Vijana na Michezo.

16. Mipango iliyokusudiwa katika utekelezaji wa malengo na madhumuni ya umoja ni:

(a) Kuanzisha na kuendesha jarida liitwalo FARAJA.
(b) Kutangaza chama na kuwaandikisha wanachama zaidr.
(c) Kuanzisha matawi.
(d) Kuendelea kupokea, kusoma na kuhariri miswada ya wanachama.
(e) Kuhimiza michango.
(f) Kufanya mikutano mara kwa mara kikatiba.
(g) Kubuni na kuendesha miradi ya uandishi, uchapaji na uchapishaji. (h) Kuendesha semina au warsha.
(i) Kuelimisha wananchi juu ya umuhimu wa kusoma, uandishi wa vitabu na sanaa zinazoambatana nazo kwa njia ya redio na magazeti.

17. Orodha ya wanachama waanzilishi:

1. L. J. Kawala

- Kigoma

2. D. Mwaware

- Dar es Salaam

3. Jumaa Mkabarah

- Muheza

4. Ali Keto

- Dar es Salaam (TRC)

5. Simon Malya

- Dar es Salaam

6. Sentore

- Dar es Salaam

7. S.K. Msuya

- Tengeru

8. Tigiti S. Sengo

- Dar es Salaam (Chuo Kikuu)

9. S. Kiango

- Dar es Salaam

10. E. Mwasada

- Dar es Salaam (Taasisi ya Elimu ya Watu Wazima)

11. J. Mbonde

- Iringa (CCM)

12. J. Rutayisingwa

- Dar es Salaam (UHURU)

13. N. Kuboja

- Mwanza

14. E. Kaungamno

- Dar es Salaam (TLS)

15. Cuthbert Omari

- Dar es Salaam

16. May Matteru

- Dar es Salaam

17. E.N. Busyanya

- Dar es Salaam

18. Penina Mlama (Bibi)

- Dar es Salaam (Chuo Kikuu)

19. Pius Ngeze

- Musoma

20. S. Shemsanga

- Dodoma

21. A. Rajabu (Bibi)

- Dodoma

22. Padre John Kabeya +

- Tabora

23. Dr. Mongi

- Tabora

24. Mchungaji Magongo

- Moshi

25. Mchungaji E.

- Morogoro

26. Hassani

- Dodoma

27. Tessua

- Dodoma

28. Miti

- Dodoma

29. Yusuf Halimoja

- Dar es Salaam

30. Ernest Ambali

- Dar es Salaam (Daily News)

31. A.H. Sakara

- Dar es Salaam (AEP)

32. L. Mtesigwa (+)

33. I.C. Mbenna

- Dar es Salaam (Taasisi ya Elimu ya Watu Wazima)

34. Amos N. Madalla

- Sokoine University

35. Euphrase Kezilahabi

- Dar es Salaam (Chuo Kikuu)

36. Mary Margareth (Bi)

- Dar es Salaam

37. Tobias Ndyeune

38. Kulikoyela K. Kahigi

- Dar es Salaam (Chuo Kikuu)

39. Joseph John Chambo

- Dar es Salaam

40. Kandaga J. Muhanga

- Dar es Salaam

41. Fatuma Friday (Bi)

- Dar es Salaam (Taasisi ya Elimu Watu Wazima)

42. S.D. Irira

- Dar es Salaam (BAKITA)

43. M. Mulokozi

- Dar es Salaam (Utamaduni)

44. Minaeli Mdundo (Bi)

- Dar es Salaam (JWTZ)

45. Estonic K.S. Monyo

- Arusha

46. Joe Mnyune

47. Alex Michael

- Mwanza

48. Makumbuli Kamtande

- Mbeya

49. Kabuterana Mbehoma

- Korogwe

50. William Nnonjela

51. Joseph J. Kasanga

- Urambo

52. Sufiani H. Shekoloa

- Mwanza

53. N.E.R. Mwakasungula

- Iringa

54. Z.M.N. Jumbe

- Dar es Salaam

55. Marseli J. Heleli

- Arusha

56. Stanslaus T.P. Bashungwa

- Mwanza

57. Hamidu Usantu

- Sumbawanga

58. Bernard Mdeka

59. Athumani J.A. Iluya

- Musoma

60. Katavo Enea Mshana

- Dar es Salaam

61. Romward Mtabi

- Dar es Salaam

62. Mac Elican Obadia

- Dar es Salaam

63. Victor C.M. Mkumbe

- Dar es Salaam

64. Evarist Njimba

- Dar es Salaam

65. John M. Wendo

- Bmga

66. Joaster T. Kisanko

- Shinyanga

67. Privatus Karugendo

68. Johnson Petro Machory

- Mwanza

68. Peter H. Kimweri

- Kilosa

70. Rashid Seif Rashid

- Pemba

71. Gaufried C. Issaya

- Songea

72. Robert Mfugale

- Dar es Salaam (Taasisi ya Elimu ya Watu Wazima)

73. Dawson Mukanda

- Dar es Salaam

74. Abdi A. Mkindi

- Usangi

75. Prophily Castory Itumbili

- Dar es Salaam

77. Erasto Z.M.Z. Mbiling'i

- Arusha

78. Mathias A.L.L. Ganyara

- Dar es Salaam

79. Enesmo N.N. Bulali

- Manyoni

80. Ansgar William Makangamko

81. Dellys K. Mihambo

- Dar es Salaam

82. Agripinus Mahanya

83. Jeff A. Okinda

84. G.S. Liwenga

- Songea

85. M.D. Sahala

- Arusha

86. Anderson Bidya

- Kasulu

87. Martin N. Katasya

- Dar es Salaam

88. M.A. Mtengula (Bi)

- Dar es Salaam

89. R. Simbakalia (Bi)

- Dar es Salaam

90. E. Mbogo

- Dar es Salaam

91. A.A. Ishabailu

- Mwadui

92. F.F. Kawegere

- Bukoba